HONGERA KWA KUOKOKA
UTANGULIZI
Karibu
kwenye Ufalme wa Mungu
Kitabu
hiki kimeandikwa kwa ajili yako. Roho Mtakatikfu amekiweka mikononi
mwako kwa kusudi muhimu la Mungu ndani ya Kristo.
Katika
Jina lile lipitalo majina yote jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi
wetu, napenda kukukaribisha katika Ufalme wa Mungu!
Imeandikwa
wazi kabisa katika kitabu cha Waefeso 2:19 ya kuwa; “Basi
tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja
na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu”.
Umepata
neema hii ya Mungu, na sasa umeokoka – biblia inakuambia tangu sasa
wewe si mgeni wala mpitaji katika Ufalme wa Mungu -
bali wewe ni mwenyeji pamoja na watakatifu wengi waliomo katika
nyumba ya Mungu!
Nia
ya Roho Mtakatifu kukuwekea kitabu hiki mikononi mwako, ni kukufahamisha
angalau kwa kiasi fulani juu ya uamuzi uliofanya wa kutubu dhambi zako,
na kumpokea Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wako.
Kitabu
hiki kitakusaidia kujua kitu gani kimetokea ulipookoka na mambo muhimu
ya kufanya katika maisha hayo mapya ya wokovu.
Umefanya
uamuzi wa busara – katika Luka 15:10 biblia inatuambia ya kuwa hata
malaika wa mbinguni wanashangilia na kuufurahia uamuzi huo uliofanya.
Na
mimi kama mtumishi wa Mungu aliye hai napenda kumshukuru Mungu katika
Kristo Yesu kwa kukufunulia siri hii ya wokovu ambayo wengi hawajaiona
na wengine wameiona lakini wanaipuzia. Ni maombi yangu kwa Mungu ya kuwa
atakutia nguvu na kukupa ufahamu wa rohoni unapokisoma kitabu hiki ili
kikusaidie katika maisha yako ya kila siku.
Christopher
na Diana Mwakasege
,
S.L.P. 2166,
ARUSHA
S.L.P. 2166,
ARUSHA
UMEFANYA
UAMUZI WA BUSARA
Umefanya uamuzi wa busara. Ndiyo! – tena ni kweli kabisa.
Umefanya uamuzi wa busara. Umeamua kutubu dhambi zako kwa Mungu, na
kumpokea Yesu Kristo moyoni mwako kama Bwana na Mwokozi wako –
umefanya uamuzi wa busara. Naamini pia ya kuwa uamuzi huu uliofanya ni
uamuzi wa kudumu.
Nimeona nikutie moyo namna hii kwa kuwa mtu anapookoka wakati
mwingine anasumbuka na mawazo na kujiuliza maswali mengi – akijiuliza
ikiwa kwa kuokoka amefanya uamuzi sahihi. Watu wengine kwa kutopata
majibu sahihi ya swali hili wanakata tamaa na kurudi nyuma kiroho – na
hata wapo wengine wanaoamua kuacha wokovu kabisa.
Nakutakia heri kwa Bwana na kumwomba Mungu azidi kujifunua wazi
zaidi kwako ili usiwe kati ya wale wanaokata tamaa na kuacha wokovu.
Umeifanya sala ya toba kwa moyo wako wote na umeokoka – ni uamuzi wa
busara mtu yeyote asikudanganye wala kukukatisha tamaa.
Umechagua
Baraka!
Umechagua kuokoka kwa kumwamini na kumpokea Yesu Kristo kama
mwokozi wako,maana yake umechagua baraka.
Inawezekana hukujua lakini mtu ambaye hajaokoka anaishi chini ya
laana, na mara anapookoka – Yesu Kristo anamtoa kwenye laana
nakumwingiza ndani yake – ambaye ndiye Baraka na chanzo cha baraka
zote za Mungu.
Tangu zamani Mungu alimpa mtu uhuru wa kuchagua kati ya baraka na
laana aliposema
“ Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana; baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya Bwana Mungu wenu…. Na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya Bwana…. (Kumbukumbu la Torati 11:26-28)
Umechagua kuokoka – umechagua baraka! Baraka maana yake, furaha, amani,
kufanikiwa, kustawi, kukua,kunawiri na kunona!
Ndiyo maana Mtume Paulo aliandika katika kitabu cha Waefeso 1:3
hivi, “Atukuzwe
Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za
rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo.”
Huu mstari unazungumza juu yako pia kwa kuwa unapookoka unaingia “ndani
yake Kristo”. Kwa kuwa ulipookoka uliingia ndani yake Kristo, kwa
hiyo umebarikiwa kwa baraka zote za rohoni!
Unaweza ukajiuliza kama ni baraka zote za rohoni je za kimwili na
za akili nitazipataje? Fahamu neno hili baraka zote zimeanza rohoni!
Ndiyo maana imeandikwa hivi katika kitabu cha Wagalatia 3:13, 14
kuwa; “Kristo
alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili
yetu, maana imeandikwa amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti, ili
kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie mataifa katika Yesu Kristo, tupate
kupokea ahadi ya roho kwa njia ya amani”
No comments:
Post a Comment